Ruka kwenda kwenye maudhui makuu

Muungano

  • Hatimaye Ethereum ya sasa itafanya "muungano" na mfumo wa uthibitisho-wa-hisa wa mnyororo kioleza.
  • Hii itaweka alama ya kuhitumu kwa Ethereum ya uthibitisho-wa-kazi, na mpito mzima kwenda kwenye uthibitisho-wa-hisa.
  • Hii imepangwa kutangulia utolewaji wa minyororo ya vigae.
  • Kabla tuliita hii hatua kama "utiaji nanga"

Ukurasa ulisasishwa mwisho: 19 Oktoba 2023

Muunganisho ni nini?

Ni muhimu kukumbuka kwamba mwanzoni, Mnyororo Kiolezaulitenganishwa na

wakati wa usafirishaji - mtandao tunaoutumia leo hii. Mtandao mkuu wa Ethereum utaendelea kulindwa na uthibitisho-wa-kazi, hata pale Myororo Kioleza utakapofanya kazi sambamba uklitumia uthibitisho-wa-hisa. Muunganisho ni pale mifumo hii miwili itakapokuwa pamoja.

Fikiria kwamba Ethereum ni chombo cha anga kilichotayari kusafiri katikati ya nyota mablimbali. Pamoja na Mnyororo wa Kioleza jamii imeunda injini mpya na ganda ngumu. Wakati ukifika, meli ya sasa itapanda gati na mfumo huu mpya, ikiungana kuwa meli moja, tayari kuweka miaka mingine mizito na kuchukua ulimwengu.

Kuunganika na Mtandao Mkuu

Wkati iko tayari, Mtandao Mkuu wa Ethereum "itaungana" na Mnyororo Kioleza, kisha kitakuwa kipande chake kinachojitegemea kinachotumia uthibitisho-wa-hisa bala ya uthibitisho-wa-kazi.

Mtandao Mkuu utaleta uwezo wa kuendesha mikataba mahiri kwenye mfumo wa uthibitisho-wa-hisa, pamoja na historia kamili na hali ya sasa ya Ethereum, kuhakikisha kuwa mabadiliko ni laini kwa wamiliki na watumiaji wote wa ETH.

Baada ya muunganisho

Hii itaashiria kumalizika kwa uthibitisho-wa-kazi kwa Ethereum na kuanza enzi ya Ethereum endelevu zaidi, rafiki kwa ikolojia ya mazingira. Kwa wakati huu Ethereum itakuwa hatua moja karibu na kufikia kiwango kamili, usalama na uendelevu ulioainishwa katika Maono ya Ethereum.

Ni muhimu kutambua kuwa lengo la utekelezaji wa unganisho ni urahisishaji ili kuharakisha mabadiliko kutoka kwa uthibitisho-wa-kazi hadi uthibitisho-wa-hisa. Waendelezaji wanazingatia juhudi zao kwenye mpito huu, na kupunguza huduma zingine ambazo zinaweza kuchelewesha lengo hili.

Hii inamaanisha huduma chache, kama vile uwezo wa kutoa ETH iliyodumu, italazimika kusubiri kwa muda mrefu baada ya muunganiko kukamilika. Mipango ni pamoja na "usafishaji" wa baada ya kuungana sasisha kushughulikia huduma hizi, ambazo zinatarajiwa kutokea mapema sana baada ya unganisho kukamilika.

Mahusiano kati ya visasisho

Visasisho vyote vya Eth2 vinahusiana kwa kiasi fulani. Kwahio tukumbushie jinsi muungano huu unavyohusiana na visasisho vingine.

Muungano na Mnyororo Kioleza

Pale tu muungano utakapotokea, wamililiki wa hisa watapewa mamlaka ya kuthibitisha Mtandao Mkuu wa Ethereum. Uchimbajihautahitajika tena kwa hivyo wachimbaji watawekeza mapato yao kwa kusimama katika mfumo mpya wa uthibitisho-wa-hisa.

Beacon chain

Muungano na usafi wa baada ya kuungana

Mara tu baada ya muungano, baadhi ya huduma kama vile kutoa ETH iliyodumu, hazitakua zinafanya kazi. Hizi zimepangwa kwa sasisho tofauti kufuata muda mfupi baada ya kuungana.

Pata habari mpya katika Kurasa za Utafiti na Maendeleo EF(opens in a new tab). Kwa wale wanaotamani kujua, jifunze zaidi kuhusu Nini Kitatokea Baada Ya Muungano(opens in a new tab), iliyowasilishwa na Vitalik katika hafla ya Aprili 2021 ETH-Ulimwenguni.

Muungano na minyororo ya vigae

Hapo awali, mpango huo ulikuwa ukifanya kazi kwenye minyororo iliyokatwa kabla ya kuungana - kushughulikia hali ya ubadilikaji. Walakini, na kuongezeka kwa suluhisho la kuongeza safu ya 2, kipaumbele kimehamia kwenye kubadilisha uthibitisho-wa-kazi kuwa uthibitisho-wa-hisa kupitia muungano.

Hii itakuwa tathmini inayoendelea kutoka kwa jamii juu ya hitaji la raundi nyingi za vipande vya minyororo ili kuruhusu uendelevu usio na mwisho.

Vipande vya minyororo

Soma zaidi

Je! ukurasa huu umekusaidia?