Ruka kwenda kwenye maudhui makuu
Change page

Viwango vya Maendeleo ya Ethereum

Ukurasa ulihaririwa mwisho: 26 Septemba 2025

Muhtasari wa viwango

Jumuiya ya Ethereum imepitisha viwango vingi vinavyosaidia miradi (kama vile wateja wa Ethereum na mikoba) iweze kuingiliana katika utekelezaji mbalimbali, na kuhakikisha kuwa mikataba mahiri na mfumo mtawanyo wa kimamlaka unabaki kuwa na utungo.

Kwa kawaida viwango huletwa kama Mapendekezo ya Uboreshaji ya Ethereum (EIPs), ambazo hujadiliwa na wanajumuiya kupitia mchakato wa kawaida (opens in a new tab).

Aina za viwango

Kuna aina 3 za EIPs:

Zaidi ya hayo, kiwango nyayo kugawa katika makundi 4:

Maelezo zaidi kuhusu aina na kategoria hizi tofauti yanaweza kupatikana katika EIP-1 (opens in a new tab)

Viwango vya tokeni

  • ERC-20 - Kiolesura cha kawaida cha tokeni zinazoweza kubadilishwa (interchangeable), kama vile tokeni za kupiga kura, tokeni za kuweka hisa au sarafu pepe.
    • ERC-223 - Kiwango cha tokeni zinazoweza kubadilishwa ambacho hufanya tokeni kuwa na tabia sawa na ether na inasaidia ushughulikiaji wa uhamisho wa tokeni kwa upande wa mpokeaji.
    • ERC-1363 - Kiolesura cha kiendelezi cha tokeni za ERC-20 kinachosaidia utekelezaji wa simurejeshi kwenye mikataba ya mpokeaji katika muamala mmoja.
  • ERC-721 - Kiolesura cha kawaida cha tokeni zisizoweza kubadilishwa, kama hati miliki ya mchoro au wimbo.
  • ERC-777 - (HAIPENDEKEZWI) Kiwango cha tokeni kinachoboresha ERC-20.
  • ERC-1155 - Kiwango cha tokeni ambacho kinaweza kuwa na mali zinazoweza kubadilishwa na zisizoweza kubadilishwa.
  • ERC-4626 - Kiwango cha kuba la tokeni iliyoundwa ili kuboresha na kuunganisha vigezo vya kiufundi vya kuba zinazotoa mavuno.

Jifunze zaidi kuhusu viwango vya tokeni.

Masomo zaidi

Unajua rasilimali ya jamii iliyokusaidia? Hariri ukurasa huu na uiongeze!_

Je! makala haya yamekusaidia?